PICHA 20 ZA MAANDAMANO YA JANA WANAFUNZI WA CHUO KIKUU CHA ST. JOHN, WALIPOANDAMANA KULALAMIKIA UBAKAJI NA MAUAJI CHUONI HAPO
| Basi mtuhumiwa huyo alichukuliwa na polisi kisha wanafunzi waliingia chuoni kuanzisha maandamano |
| Hapa walikusanyika kwenye bendera kisha kuongea na mkuu wa chuo |
| Mkuu wa chuo alisema pia nao wamechoshwa na mambo mabaya ambayo wanafunzi wanafanyiwa. Hivyo wanafunzi wawe na subira wanafanya taratibu za kibari cha maandamano ya amani |
| Wanafunzi baada ya kusubili kwa muda mrefu kibari icho wakaamua kuandaa mabango kwa ajili ya maandamano, ambapo kibari kipatikane kisipatikane walidai kuandamana ni lazima |
| Basi wanafunzi wakaanza kuchora mabango yao kwa ajili ya maandamano |
| Mabango yalipokamilika wakasimama kwenye bendera kwa mara nyingine |
| Walifika mbali na kuona kuwa polisi wanahusika katika mambo mabaya wanayofanyiwa. Ndipo wakachora bango hili kuonyesha hisia zao |
| Wakaamua kuingia barabarani kwa maandamano baada ya kujaa munkari na jaziba kubwa |
| Hapa wapo barabarani na masomo kwa siku ya leo hayakuwepo |
| Bango lina picha ya mwanafunzi alieuliwa kikatili, aliefahamika kwa jina la LYDIA LEO |
| Ni mchaka mchaka ulioendana na nyimbo za hisia |
| Magari yalisimama kwa muda mrefu mjini hapo mpaka wanafunzi walipomalizika kupita, kwa hiyo wenye haraka walichelewa |
| Haya huyu anaashiria demokrasia na maendelea ndio imetawala juu yao |
| Msafara hapa unaelekea maeneo ya Bungeni |
| Kila walipopita walikuwa wakishindikizwa na polisi kuhakikisha amani inatawala |
| Gari la maji ya kuwasha lilikuwepo lakini wanafunzi hao hawakutishika na kitu chochote kile kutoka kwa Polisi |
| Wanafunzi walifika mpaka Nyerere Square waliimba nyimbo mbalimbali mahala hapo |
| Baada ya kutembea mji mzima na mabango yao na kuhakikisha kiu yao imekwisha basi waliamua kurudi chuoni |
| Gari la washa washa nalo lilikuwepo lakini watu walikuwa na jaziba zao vilevile mwanzo mwisho |
| Barabara zilikuwa zimetawaliwa na wanafunzi kwa kiasi kikubwa, mpaka kusababisha magari kutopita |
| Hapa ilibidi nipande gari la polisi ili niweze kuchukua picha vizuri, sio siri polisi wenyewe walikuwa wamechoka kwa kutembezwa mji mzima baada kuchat nao kwenye gari ilo |
| Hapa ndipo safari ya maandamano ilipoanzia na ndipo safari hiyo ilipoishia maeneo haya ya kwenye bendera mbele ya jengo la administration. |
No comments:
Post a Comment