Monday, January 28, 2013

TEJA AKUTWA AMEKUFA KWA KUJIDUNGA MADAWA YA KULEVYA

Nyumba ambayo mwili  huo umekutwa
mwili  wa kijana Stan Mhepelwa ukiwa katika gari ya polisi leo
Bomba la sindano lililokutwa katika chumba  hicho
Mwili  wa kijana  huyo ukitolewa

Kijana anayesadikika kuwa mtumiaji  wa madawa ya  kulevya (teja) mjini Iringa Stan Mhepelwa  mkazi  wa Ilala katika Manispaa ya Iringa amekutwa akiwa amekufa katika  nyumba  ambayo bado  kukamilika eneo la barabara  mbili katika Manispaa ya Iringa.

Mashuhuda wa  tukio  hilo  wameueleza mtandao  huu wa www.francisgodwin.blogspot.com  kuwa  tukio  hilo  limetokea  usiku  wa kuamkia leo  jumapili ambapo  mwili  wa  kijana  huyo  umekutwa  mida ya saa 3 asubuhi  na  wananchi  waliokuwa  wakipita  eneo  hilo .

Samson Kalinga ni mkazi  wa  eneo  hilo amesema  kuwa  nyumba  hiyo imekuwa  ikitumiwa na vijana hao mateja kama  sehemu ya  kujificha na kujidunga madawa  ya  kulevya kwa  kutumia sindano na kuwa  chanzo  cha kifo cha kijana  huyo kinasadikika kuwa alijidunga sindano  vibaya .

Hata  hivyo  alisema mwili  wa  kijana huyo umekutwa katika  chumba  hicho huku pembeni  kukiwa na mabomba ya sindano na kuwa aliyetoa siri ya  kifo cha kijana  huyo ni teja mwenzake ambae  alikuwa akiingia katika  chumba  hicho ili kuendelea  kutumia madawa  ya kulevya.

No comments:

Post a Comment