OMBA OMBA IRINGA WAJA NA MBINU MPYA YA 'KIDIGITALI' KATIKA KUOMBA ,SASA WASHINDA KTK ATM
Hapa mteja huyo akitoka huku omba omba huyo akimwomba pesa .
WATU wanaofanya kazi ya omba omba katika manispaa ya Iringa mkoani Iringa wamejigungulia mbinu mpya ya kuomba pesa kwa watu mbali mbali baada ya kuona kasi ya wananchi kuwasaidia kupungua na idadi ya omba omba ikiongezeka na hivyo ili kupambana na wale wenye tabia ya kusema sina pesa ,sasa omba omba wameamua kukaa maeneo yenye mashine za kutoa fedha (AMT ) ili kufanya shughuli hiyo.
Mmoja kati ya omba omba maarufu mjini Iringa ambae hakupenda kutaja jina lake alisema kuwa wameamua kubuni mbinu hiyo baada ya wananchi nao kubuni mbinu ya kuwanyima pesa kwa kila anayeomba fedha hata kama mfukoni ana pesa bado amekuwa akiwanyima kuwa hana pesa.
" Tumeamua kuboresha huduma yetu zaidi kuhama katika mfumo wa zamani ya analojia na kujiunga na mfumo mpya wa Digitali kwa kusogea katika mashine za ATM kama unavyoona sasa wengi wetu tunawasubiri wasamaria wema katika mashine" alisema mwanamke huyo
Hata hivyo alisema sababu nyingine ya kuondoka barabarani ambako awali walikuwa wakijipanga kuomba fedha ni kutokana na idadi ya omba omba kuongezeka zaidi katika barabara mbali mbali za mji wa Iringa hivyo kukosa fedha ya maana na wengi wao kujikuta wakirejesha majumbani kwao bila kupata hata senti moja.
Alisema kuwa mbinu hiyo ya kusogea katika mabenki ya katika mashine za ATM umeanza kuzaa matunda kwao kutokana na sehemu kubwa ya omba omba kutojua kusoma hivyo wamekuwa hawajui kama katika mashine hizo ndiko watu wanakotoa fedha hivyo kwa wale wajanja wamekuwa wakipata zaidi kwa kuwafuata watumiaji wa ATM katika maeneo husika .
"ujue mwanangu hapa katika ATM mtu kukunyima anaona aibu kwani tayari umemwona anachukua pesa na pili hawezi kukupa chenji chenji kwani mashine hizi hazitoi chenji ....ila ukikaa barabarani wanakupa shilingi 50 ama 100 sasa unaweza kutwa nzima ukashindia 2000 wakati hapa katika ATM unaweza kupata hadi shilingi 50,000 kwa siku .....sasa anglia mwenyewe wapi panafaa" alihoji omba omba huyo.
Wakati omba omba hao wakionyesha ubunifu mkubwa katika kazi hiyo baadhi ya wananchi wa Manispaa ya Iringa wameutaka uongozi wa Manispaa ya Iringa na mkoa kuigilia kati suala la kuongezeka kwa omba omba hao na kuwa wapo baadhi ya watu wamekuwa wakidanganya kama ni omba omba kumbe wa watu wenye familia zenye uwezo .
Huku baadhi yao wakiingiza kuwa ni walemavu wa viungo kumbe ni matapeli wanaoigiza ulemavu ili kujipatia fedha na wanaponyimwa fedha wamekuwa wakiwatukana wale wanaowanyima matusi ya nguoni ama hata kutaka kuwapiga.
No comments:
Post a Comment