HACKER MAARUFU GEOHOT AAJIRIWA NA FACEBOOK
Geohot,
hacker maarufu aliyejailbrake iPhone ameajiriwa rasmi na Mark
Zuckerburg, yaani Facebook. Hacker huyu ambaye pia aliwahi kushitakiwa
na Sony kwa shughuli za uchakachuaji baada ya kuihack PS3 na kuruhusu
watumiaji kuweza kutumia DVD feki za kuchakachua. Facebook
hawakuthubitisha Geohot atafanya kazi gani kwenye kampuni hiyo. Hacker
huyu ambaye anatumia majina mbali mbali katika shughuli zake pevu ikiwa
ni pamoja na million75, mil, dream na hax0r ameshafanya fujo nyingi sana
katika ulimwengu wa kompyuta. Kijana huyu kwa sasa ana umri wa miaka 22
tu.
Jina
alilopewa na wazazi wake ni George Francis Hotz. Katika kazi za
karibuni kabisa alizofanya hacker huyu ni kujailbraik iPhone na iPod
Touch kwa kutumia njia aliyoiita Blackra1n na pia kuifungua (sim unlock)
simu hiyo kwa njia aliyooiita blacksn0w.

No comments:
Post a Comment