Friday, November 30, 2012

WATU WANNE WALIYOMUIBIA NGUO NA KUMKATA VIDOLE SHARO MILIONEA WAKAMATWA....

Watu wa nne wamekamatwa na jeshi la police wakiwa na Baadhi ya vitu alivyokuwa navyo marehemu Sharo Milionea kama vile Jeans,T-Shert,Viatu,Simu ya mkononi,Pete,Cheni,Tairi moja la gari,pamoja na Battery la gari alilopatanalo ajali marehemu Sharo Milionea....Inasemekana watu hao waliposhindwa kumvua Pete vidoleni walimkata vidole vyake....Watuhumiwa hao walikuwa sita wamekamatwa wanne bado wawili waliokimbia na pesa alizokuwa nazo Maremu Sharo Milionea....

Wednesday, November 28, 2012

  1. CHUKUA TAHADHARI KABLA HATARI

Habari ya kweli iliyotokea wiki iliyopita.
Kuna dada mmoja anasoma chuo buguruni na pia ni mfanyakazi hivyo jioni akitoka kazini ndipo huenda shule.Sasa akiwa njiani kuelekea chuo akapigiwa simu na mtu asiyemfahamu akajitambulisha kwamba yeye ni daktari wa lugaro hosp na kumuulizia habari za mwanae ambae alishawahi kwenda kumtibu pale na chakushangaza zaidi akataja mpaka aina na rangi ya nguo aliyovaa siku ile alipokwenda hapo hospitali na yote yalikuwa kweli.
 Na zaidi akamwambia najua sasa hivi unaelekea chuo buguruni na kweli ilikuwa hivyo, lakini mwishoni akamweleza kwamba kuna mambo anataka kujua kujua kuhusu hicho chuo hivyo nae anaelekea huko hivyo akifika tu atamtafuta. Kwa muda wote huo huyo dada hakuweza kabisa kumkumbuka ila akajipa moyo kwamba yamkini huyo mtu atakuwa  anamfahamu vizuri.
Baada ya kutoka chuo akiwa na wenzake watatu akawa anawasimulia habari za huyo mtu ndipo simu yake ikaita,kupokea yule mtu akamwambia nakuona uko na wenzio wawili mnavuka barabara na kumueleza jinsi alivyovaa sasa wenzie wakasema huyo mtu anakufahamu haiwezekani hapa tupo watatu kweli na ameweza kukutambua. Kisha huyo mtu akamwelekeza mahali alipo ambapo haikuwa mbali na barabara.
Lakini alipomtazama hakumfahamu kabisa, basi akampa mkono kumsalimia, baada ya hapo hakujitambua na zaidi alijikuta yuko maeneo ya chuo kikuu cha DSM akiwa hoi. Kuangalia simu na kila kitu chake kilikuwa salama na hakufanyiwa kitu chochote, kwa bahati kulikuwa kuna ndugu yake anasoma chuo hivyo akawasiliana nae ili kupata msaada ikabidi awahishwe mwananyamala hosp lakini ikaonekana sumu iliyotumika ni kali na dawa yake wanayo regency hosp,hivyo akawahishwa regency na kupata matibabu.
Baada ya ufahamu kumrudia akakuta mtu huyo kachukua pesa zote kwenye mpesa,tigo pesa na bank ( NMB na CRDB) kiasi cha milioni 3, hivyo inawezekana walipompa sumu alitaja password pasipo kujijua.
Na bank walipotazama kwenye ATM Camera waliona picha ya huyo mtu na yeye alimkumbuka vizuri, lakini polisi Kijitonyama wakakiri kwamba kesi hizo sasa hivi zimetokea mara nyingi na huo mtandao ni mkubwa, walipoenda kwenye usajili wa simu walikuta ni huyo huyo na jina lake ndilo alilojitambulisha.Ingawa polisi wameshindwa kumkamata.
Akiwa kituo cha polisi mara huyo mtu akampigia simu akimwambia ‘’kumbe wewe ni muoga sana tutakurudishia pesa zako’’. Sasa kumbe wanachofanya wanakuambia’’ tutafutie mtu ambae unahisi ana pesa kuliko hizi  halafu tukifanikiwa tutarudisha pesa zako’’ hivyo inawezekana nae kuna mtu anaemjua alifanyiwa hivyo akaamua kumtaja yeye

Tuesday, November 27, 2012

DIAMOND ASHINDA TUZO ZA ZUMARI MSANII BORA WA KIUME









ALBUM 25 KALI ANAZOZIPENDA WIZ KHALIFA


1996 (25) 2004 (24) 1997 (23) 2006 (22) 21 (2003) 20 (2009) 19 (2002) 18 (2000) 17 (2000) 16 (2005) 15 (2009) 14 (2010) 13 (2003) 12 (2001) 11 (1998) 10 (1994) 9 (2002) 8 (2003) 7 (1996) 6 (2000) 5(1998) 4 (1993) 3 (1998) 2 (1998) 1 (1993) its more about music industry and social issues in and out of

ALBUM 25 KALI ANAZOZIPENDA WIZ KHALIFA


1996 (25) 2004 (24) 1997 (23) 2006 (22) 21 (2003) 20 (2009) 19 (2002) 18 (2000) 17 (2000) 16 (2005) 15 (2009) 14 (2010) 13 (2003) 12 (2001) 11 (1998) 10 (1994) 9 (2002) 8 (2003) 7 (1996) 6 (2000) 5(1998) 4 (1993) 3 (1998) 2 (1998) 1 (1993) its more about music industry and social issues in and out of

BREAKING NEWS: MSANII SHARO MILLIONEA AFARIKI DUNIA


Msanii wa Bongo movie na mwanamziki Sharo milionea amefariki dunia leo hii kwa ajali ya gari alipokua akielekea Muheza, Tanga., kwa habari zilizothibitishwa na msanii mwenzake wa movie Steve Nyerere, akiongea akiwa katika msiba wa msanii mwingine wa Bongo movie alifariki (John) kwa njia ya simu, akisikika kwa sauti ya masikitiko sana alisema
"ni kweli fetty sharo hatupo nae tena na nimeongea na kamanda wa polisi mkoa wa Tanga na kuthibitisha habari hizo"
 akiongea na Clouds Fm, kamanda wa polisi mkoa wa Tanga Bwana Constatine Massawe amesema " kifo cha Millionea kimetokea majira ya saa mbili, eneo linaloitwa Maguzoni songa , akiwa anaendesha gari aina ya toyota Harrier akitokea Dar  kuelekea Muheza, alipofika hapo gari liliacha barabara na kupinduka,na maiti imehifadhiwa katika chumba cha maiti ya  hospitali teule ya Muheza. alikuwa mwenyewe. Mungu ailaze roho ya marehem mahali pema peponi Amen
hii ni moja kati ya kazi alizowahi kuzifanya katika uhai wake 

HUU NI UJUMBE KUTOKA KWA MAREHEMU BAADA YA KU CHART NA LINEX


Huu ni ujumbe kutoka kwa marehemu baada ya ku chart na msanii wa* Bongo Fleva *hapa Tzee almaarufu kama Linex Sunday.Sasa ebu sikiliza ujumbe mwingine kutoka kwa Bw.Seif Makame hapo chini. its more about music industry and social issues in and out of bongo

KWA MUJIBU WA MO NA GASTAR KUTOKA CLASSIC RECORD


Baada ya kutokea kifo cha msanii almaarufu Sharo milionea ,sasa kwa namna moja au nyingine wasanii mbalimbali na watu wote tumeguswa na msiba huu.Kwa mujibu wa producer Mona gastar leo asubuhi aliweza kuniambia kwamba studioni kwake kuna baadhi ya wasanii waliojitokeza kuja ku record ngoma kwa ajili ya kumuenzi Sharo Milionea.Baada ya hapo ndipo nikaona ujumbe kutoka Country Boy kupitia katika ukurasa wake wa Facebook huu hapa. its more about music industry and social issues in and out of bongo land

ALICHOKISEMA KITALA KABLA MAREHEMU SHARO MILIONEA AJAFA HIKI HAPA


*Baada* ya kutokea kifo cha *Sharo Milionea* jana huko Tanga,kiukweli tumepoteza mtu ambaye mwenye vipaji vizuri vya kuelimisha jamii,sasa hapa nina rafiki yake wa karibuni sana anaelezea jinsi walivyoacha na mauti kumkuta.*R.I.P Sharoo* its more about music industry a

Thursday, November 22, 2012

P FUNK AFUNGUKA KUHUSIANA NA MIPANGO YAKE KATIKA GAME

Kama ulimiss kusikiliza 255 ya Deeandy leo kuhusiana na P Funk alichokizungumza kuhusu na kiwango cha muziki hapa Tzee,basi hii ndiyo time yako ya kusikiliza kile ambacho achokisema kuhusiana na mipango yake katika muziki wa hapa Bongo.

AFANDE SELE AIRUDISHA TENA WATU PORI KWA KASI ZAIDI

 Msanii wa Bongo Fleva kutoka mji kasoro bahari Morogoro almaarufu kama Afande Sele anayekubalika kwa mashabiki hata kwa wasanii wenzake kwa kutoka na utunzi wake wa mashairi mazuri,sasa latest info kutoka kwa Afande Sele ni kwamba leo ameachia ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la "Amani na Upendo" akiwa na Koba MC.Baada ya hapo kupitia katika ukurasa wake wa Facebook aliweza  kuandika huu ujumbe baada ya kuiachia ngoma hiyo mpya.

Saturday, November 17, 2012

A .Y ANYAKUA TUZO YA KWANZA USIKU HUU

 Msanii wa Bongo Fleva almaarufu kama  A.Y leo huko nchini South African amejichukulia tuzo ya kwanza katika kipengele cha Most Gifted East African video of the Year na hii ndiyo list ambayo alikuwa akichuana nayo katika kuwania tuzo hizo
Most Gifted East African video of the Year

  • Keko Feat. Madtraxx – Make You Dance
  • Camp Mulla – Party Don’t Stop
  • AY feat Sauti Soul – I Don’t Want To Be Alone
  • K’Naan Feat. Nas – Nothing To lose
  • Navio – One & Only

Wednesday, November 14, 2012

HUU NDIO UJUMBE KUTOKA KWA TIGO BAADA YA KUTO KUPATIKANA KWA HUDUMA YAO LEO ASUBUHI


Hiki ndicho walichokiandika Tigo leo kupitia katika ukurasa wao wa Facebook na kuwaomba radhaa Wananchi baada ya mtandao wao kutokufanya kazi kuanzia Asubuhi na kupelekea watu kukosa huduma zao.Sasa pale comment zilipozidi kuwa nyingi katika page yao huku watu wakilalamika kuhusiana na huduma zao sasa wakaamua ku upadate ujumbe mwingine huu hapa chini.
Baada ya masaa mawili ndipo huduma zikaanza kufanya kazi na wakatoka ujumbe huu hapo chini

DJ CHOKA SOON KUACHIA ALBUM YAKE MPYA

Ni moja kati ya watu wenye umaarufu fulani hapa Tzee kwa kupitia kazi za wasanii mbalimbali katika media au pale mtu anapokuwa na kazi yake basi lazima ukutane na huyu mtu hata support kazi yako kwa kupitia blog yake sasa
Latest info kutoka kwa Dj Choka mrApetite ni kwamba kwa sasa yuko mbio kwa kuachia album yake mpya  siku ya tarehe 12 mwezi wa 12 pia baada ya kusema hivyo alimaliza kwa kusema kwamba baada ya ngoma inayofahamika kwa jina la  Pamoja we Can.Mashabiki wakae tayari kwa ujio wa ngoma mbili mpya za kwake kwa mpigo.@info kamili Dj choka Mr Apetite.

MWANA FA YUKO STUDIO HIVI SASA AKIANDAA NGOMA YAKE MPYA

Msanii wa Bongo Fleva almaarufu kama Mwana FA baada ya kutamba na ngoma kali kama Yalaiti,Nangoja Ageuke,Unanijua unanisikia,Bado nipo nipo sasa
Latest Info tumezipata hivi sasa ni kwamba msanii huyu hivi sasa  yuko ndani ya Bongo Record akifanya ngoma yake mpya na Mafumu Bilali lakini hakuweza kusema  ni ngoma gani ila alisema atafanya suprise kwa mashabiki wake.Hiyo ndiyo picha ambayo akiwa studio aki record ngoma yake mpya ambayo soon anatarajia kuachia..!!!!!!!

MANECKY SOON KUFANYA KAZI NA TOP 5 WA EPIQ BSS BURE

Ni moja kati ya ma producer wakali hapa Tzee baada ya kufahamika kwa touch zake mbalimbali alizozifanya hapa Tzee kama Nataka Kulewa,Hakunanga,Demu sio n nyinginezo kali sasa
Latest info kutoka kwa Producer huyu ni kwamba siku za hivi karibuni baada ya washiriki wa Epiqbss kuonyesha vipaji vyao siku ya Fainali ilyofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee sasa Manecky amejitolewa ofa kwa washiriki waliongia Top 5 kwa kufanya kazi katika studio yake bure.baada ya kusema hivyo alimalizia kwa kusema kwamba mashabiki wa Walter na washiriki wengine kaeni kwa ujio mpya wa wasanii hao

R.I.P MARIAM KHAMIS

 Msanii wa taarab nchini Tanzania wa kundi la TOT plus, Mariam Khamis almaarufu kama paka mapepe amefariki dunia usiku wa jana kuamkia leo katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam mara tu baada ya kujifungua .

Mariam Khamis umauti umemkumba akiwa anaimba kundi la TOT plus lakini enzi za uhai wake aliwahi kuimbia katika makundi mbalimbali ya taarab likiwemo East Africa Melody, Zanzibar Stars na 5 Stars.

Khamis Muhidini Shomary baba wa marehemu amesema mipango ya mazishi inaendelea kufanyika ambapo anatarajiwa kuzikwa hapo kesho Magomeni Kota jijini Dar es Salaam.info kamili baba mzazi wa Mariam Khamis.

NU JOINT: TUTAONEKANAJE / WANAUME TMK

 
Download na usikilize exclusive wimbo mpya kutoka kundi la Wanaume Tmk Family unaoitwa Tutaonekanaje ukiwa umefanywa na producer/Msanii Shirko



LADIES AND GENTLEMAN: HII NI HIT NYINGINE KUTOKA KWA ALI KIBA / MY EVERYTHING

Unakumbuka kuna story flani zilitoka kuwa mtu mzima Ali kiba soo atakuwa chini ya Sonny Music kama mwanadada Keko kutoka Uganda, sasa fununu nilizonazo ni kuwa jamaa kasha saini mkataba na Sonny.. na hii ni relese yake mpya na trust me kwa nilivyoisikiliza lazima ibambe.
sikiliza hapo chini kitu kinaitwa "my everything "

Monday, November 12, 2012

FID Q AJA NA IDEA MPYA KWA MASHABIKI WAKE

Msanii wa Bongo Fleva anayeondoka Style za HipHop almaarufu kama Fid Q msanii wa Ladha kali za Hip Hop anayesababisha mpaka mashabiki kupenda ngoma zake kama ielewe mitaa,Propaganda,Neno,na zinginezo kali sasa
Latest Info kutoka kwa Fid Q ni kwamba sasa hivi alichoamua kufanya kwa mashabiki wake ni kwamba ameona atakuwa anatoa cover ambazo zitakuwa zina mashairi yake HipHop kwani alieleza kwamba kutokana mashabiki wengi pamoja na ma Professor wa Vyuo Kikuu kukubali kazi zake na ndiyo sababu kubwa mpaka kuchukua uamuzi huo wa kutoa cover ambazo zitakuwa na mashairi yake kama hiyo hapo juu.

DIAMOND AGUNDUA KITU BAADA YA WALTER KUWA MSHINDI WA EPIQ BSS

Msanii wa kizazi kipya hapa Tzee almaarufu kama Diamond Platinum wa wasafi baada ya kutamba na ngoma zake kali na kupelekea kuwa na mashabiki wengi hapa Africa sasa
Latest Info kutoka kwa msanii huyu ni kwamba leo kupitia katika mtandano wake ameweza kuandika kwamba amegundua kitu kwa msanii wa Epiq Bss baada ya kutwaa ushindi na huu ndiyo ujumbe kutoka katika mtandano wake unaojulikana kwa jina la This is Diamond huyu hapa anafunguka kama hivi"Kiukweli muda wangu uwa ni mchache sana kukaa kwenye TV,ila siku ambayo Walter aliimba wimbo wa Mawazo nilikuwa home.....nikamsikiliza kwa umakini sana nakugundua anakitu ndani yake, namaanisha ana uwezo wa ziada na nafasi nzuri katika muziki wa Tanzania, swala la kufika level za kimataifa hilo ni swala la sisi watanzania kumwezesha pamoja na Yeye kuwa under management makini hasa kipindi hichi anachoanza kuingia katika fani hii ya muziki....nilimpigia kula nikijiamini Walter ndiye mshindi wangu na kweli hajaniangusha....Nimefurahi sana. Nakutakia kila La Heri.Huo ndiyo ujumbe kutoka kwa Diamond baada ya kumkubali Walter.

Sunday, November 11, 2012

CHECK OUT:WAKILI WA LORD EYEZ AKIFUNGUKA KUHUSIANA NA KESI INAYOMKABILI MSANII HUYO KWA TUKIO LILILOTOKEA SIKU ZA HIVI KARIBUNI

Msanii wa Bongo Fleva kutoka A town city almaarufu kama Lord eyez ambaye siku za hivi karibuni alikabiliwa na kesi ya kuiba vifaa vya gari sasa
Latest Info ni kwamba msanii huyu pamoja na Wakili wake waliamua kuweka wazi juu ya kesi inayomuanda hivi sasa.Wakili huyu anayekwenda kwa jina la Peter Kibatala alisema kwamba kesi hii imefanya mpaka Lord Eyez kuonekana kwamba yeye ndiyo mhusika wa kuiba vifaa hivyo lakini sasa hivi wanaachia kwanza Mahakama ndiyo itakayo chukua uamuzi sahihi kuhusiana na kesi hiyo.Lakini hapo hapo tuliweza kusikia ujumbe kutoka kwa weusi walizungumza na kusema kwamba tukio kama ili limewaathiri pale wanapokutana na watu mbalimbali na kusikia story za watu kusema kwamba wote watakuwa wanahusika katka kesi hiyo wakati ni story ambazo sio za kweli.Baada ya hapo tuliweza pia kusikia ujumbe kutoka kwa Lord Eyez mwenyewe  aliweza kuzungumza kusema kwamba mahakama ndiyo itaamua kuchukua sheria kwamba alihusika au ajahusika katika tukio kama hilo la kuiba vifaa vya gari,ambayo kesi hiyo inatarajia kusomwa Mahakama ya Mwanzo siku ya tarehe 13,14 na 15 mwezi huu hapa jijini Dar es Salaam lakini pia alimalizia kwa kusema japokuwa  kwa sasa hivi yupo kitaani huku akisikilizia  Mahakama imeamuaje kwa hiyo anachotaka kukifanya ni anataka kudondosha ngoma yake mpya kali ambayo anataka kufanya suprise kwa mashabiki wake katika industries hii ya muziki wa Bongo Fleva.

                                                                     Lord Eyez
                                                                      Nikki wa Pili
                                                                         G nako
                                                        Lord Eyez akiwa na wakili wake

                                                                        Weusi!!!!!!!!!

BEN POL AWATEMA OGOPA VIDEO KATIKA KUFANYA VIDEO YAKE MPYA"PETE"

Msanii wa Bongo Fleva almaarufu kama Ben Pol anatamba na ngoma kadhaa kali za RNB kama Nikikupata,Samboira,Pete, na ngoma zingine kali alizopewa collabo hapa Bongo sasa.
Latest info kutoka kwa Ben pol  kama unakumbuka kipindi cha nyuma alishawahi kuzungumza kwamba video yake mpya ambayo inakwenda kwa jina la Pete alikuwa anatarajia kwenda nchini Kenya kuifanya shooting  na Production ya Ogopa
Sasa leo baada ya kupiga naye Story za hapa na pale ameamua kutiririka na kuweka wazi baada ya kumuliza vipi kuhusiana na video hiyo alisema kwamba ameamua kufanya na Adamu Juma kwani Director huyu ametokea kumkubali baada kufanya powa video yake inayofahamika kwa jina la Nikikupata.Baada ya kumaliza kusema hivyo pia aliamua kusema kwamba Jumapili inayokuja ndiyo anatarajia kuanza shooting na Director Adamu Juma kutoka Next Level.@Info kamili by Ben pol Artist.

Friday, November 9, 2012

DIAMOND AFANYA NGOMA MPYA NA DULLY "UTAMU"

Msanii wa Bongo Fleva almaarufu kama Diamond wa wasafi baada ya kuachia ngoma yake mpya inayofahamika kwa jina la Nataka kulewa sasa
Latest info kutoka kwa msanii huyu ni kwamba ameweza kufanya ngoma nyingine ambayo amepewa collabo na Dully Skyes chini ya Producer  P funk kutoka Bongo Records.Baada ya kumaliza kufunguka kuhusiana na collabo hiyo mpya alisema kwamba ni moja kati ya collabo ambayo alikuwa anaisubiri sana na hatimaye wameshamaliza ku record na siku za hivi karibuni inaweza ikatoka.
Check out hapo Diamond akiwa zake ndani ya Bongo Record akifanya vitu vyake sasa hii ni nomaa!!!!!

A.Y AONGELEA KUHUSU MAFANIKO YAKE MWAKANI

Msanii wa Bong Fleva almaarufu kama A.Y baada ya kutoa ngoma yake inayofahamika kwa jina la Money Money aliyofanya na mwanadada Vanessa Mdee na kupeleka mpaka mashabiki kuendelea kumkubali katika tasnia hii ya muziki sasa
Latest info kutoka kwa A.Y aliweza kueleza focus yake katika mwaka unaokuja alisema kwamba anachotaka kukifanya yeye ni ku focus zaidi kazi zake ziweze kufika mbali Hapa Africa hata nje ya Africa baada ya kusema hivyo alisema kwamba kuna baadhi ya ngoma zake ambazo ameziandaa kwa ajili ya mwaka unaokuja kama kuna collabo aliyofanya na P Funk,Fid Q,Chid Benz na wengineo.@info by A.Y

LORD EYES MWANASHERIA KUONGEA NA WAANDISHI WA HABARI KESHO KATIKA HOTELI YA WISTAZ SINZA

Kesho ni siku ambayo yale maswali mengi tuliyokuwa tunajiuliza kuhusu Tuhuma za wizi wa Power window zinazomuhusisha msanii kutoka katika kundi la Weusi Lord Eyes, zitapata majibu pale ambapo Lord Eyez alienda nje kwa dhamana akiwa na mwanasheria wake wataongea na waandishi wa habari katika hoteli inayoitwa Wistaz iliyoko sinza kuanzia saa tano asubuhi  na kuelezea mkasa wote  na kinachoendelea kwa sasa

VIDEO HII YAPIGWA MARUFUKU


video ya single mpya ya Pitbull inayoitwa " dont stop the party" imepigwa marufuku kuchezwa kwenye television za UK baada ya kuonekana kutokuwa na picha nzuri kwa vijana kwa kuwa na vipande vyenye kuonyesha picha zisizofaa

inasemekana video hiyo imepatikana na makosa 25 yaliyokeuka sheria na hivyo kunyimwa airtime katika tv za UK....  video yenyewe itazame hapo chini

TUNDA AMMWAGIA MICHOZI MTOTO WA KIKE?????????

Inasemeka Tundaman aonekana akimpigia magoti dem na kummwagia michozi dada yetu,na licha ya kufanya hivyo lakini hakufua dafu kwa mwanadada.

MAMA AJIFUNGUA OBAMA NA MITT ROMNEY

 
 Millicent Owuor akiwa amewabeba watoto wake wawili wakiume mapacha Barack Obama (kushoto) na Mitt Romney.

Mwanamke mmoja kutoka Siaya kenya amejifungua watoto mapacha wawili siku ambayo Obama alichaguliwa kwa mara ya pili kuendesha taifa la Marekani kama Raisi na kuwapa watoto wake majina yake na mpinzani wake Mitt Romney 
Millicent Owuor mwenye miaka 20  alijifugua watoto hao mapacha  katika hospitali ya wilaya ya  Siaya umbali kidogo kutoka katika kijiji walichoishi mababu zake na Obama kinachoitwa Kogelo ambapo sherehe za kumpongeza Obama zilikua zikiendelea