Friday, September 27, 2013

                                  

                                            TAHADHARI TAHADHARI TAHADHARI  KWA WAKAZI WA IRINGA....................................kumeingia wizi mdogomdogo wa simu ambao unajitokeza katika manispaa ya iringa.....kijana mmoja anayefahamika kwa jina la DAVID LAWA amekua kidokozi wa simu za mikononi katika maofisi na sehemu mbalimbali anavyokua muonekano wake ni mtanashati vizur na mwisho wa siku anakuomba simu ampige na kusema anaacha  mizigo yake....na ukija kuangalia akiwa ameondoka unagundua ni mawe kwa hiyo kijana huyo anatafutwa na jeshi la polisi iringa kwa  msaada wa picha yake ni hiii hapa chini

                                         
KWA MSAADA PIGA NAMBA...........0767115584..................ASANTENI

TAFADHALI UKIPANDANDA BODABODA EPUKA SANA KUENDESHWA KWA MWENDO WA KASI, TAZAMA PICHA ZA AJALI MBAYA ILIYOTOKEA JANA MAENEO YA MANZESE MWEMBECHAI. {PICHA ZINATISHA}




WANANCHI WAKIANGALIA MWILI WA MAREHEMU


MWILI WA DEREVA BODABODA AJALI MBAYA SANA LEO IMESHUHUDIWA NA HABARI24 MAENEO YA MANZESE MWEMBECHAI AMBAPO DEREVA BODABODA AMEGONGWA VIBAYA NA KUFARIKI HAPO HAPO NA DALADALA








HII NDIO GARI ILIYOMGONGA DEREVA BODABODA MAENEO YA MANZESE

Tuesday, September 24, 2013

PICHA:KIGOGO WA TRA AMWAGIWA TINDIKALI,AWA KIPOFU..ALIA NA SERIKALI

*Sasa ni kipofu, adai serikali imemtelekeza Na Richard Konga, Arusha
TINDIKALI inaweza kuwa silaha hatari sana na haifai hata kidogo katika jamii, wanaokutwa nayo ingefaa wafungwe kifungo cha maisha kwani wanapoitumia vibaya huleta madhara yasiyoelezeka.

Elisha Kombe kabla na baada ya kumwagiwa tindikali.
Kuthibitisha hayo tunawaletea maelezo ya Elisha Kombe aliyekuwa Afisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),Kitengo cha Upelelezi mkoani Mwanza, aliyemwagiwa tindikali akiwa katika majukumu ya kikazi mkoani humo.
Miaka 15 iliyopita alikuwa mchapakazi na tena mtanashati na nadhifu mwenye viungo kamili na alikuwa akifanya kazi yake kwa umakini mkubwa lakini leo, anaililia serikali kwa kile alichodai kumtelekeza baada ya kumwachisha kazi kutokana na tukio hilo lililomfanya awe kipofu.
Kombe alikutana na mwandishi wetu mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Arusha ambapo anaishi na kaka yake, George Kombe baada ya kunusurika kifo kutokana na kumwagiwa tindikali wakati alipokuwa Mwanza kwa shughuli maalumu za kikazi.
Akisimulia mkasa huo wa kumwagiwa tindikali, Kombe alisema: “Nilipata uhamisho kutoka Makao Makuu ya Mamlaka ya Mapato Tanzania Dar es Saalam (TRA)  Septemba, 1997 kwenda mkoani Mwanza kwa ajili ya kazi maalumu ya ukaguzi na kudhibiti mianya ya ukwepaji wa mapato na magendo kwa baadhi ya wafanya biashara wasio waaminifu.
“Nikiwa Mwanza nilishuhudia mianya hiyo ya ukwepaji wa mapato kwa baadhi ya wafanya biashara waliokuwa wakitumia usafiri wa majini na baadhi ya meli na boti zilikuwa zikisafirisha bidhaa kwa njia isiyo halali sambamba na magari yaliyokuwa yakitumika nchi kavu.
“Pamoja na upinzani niliokuwa naupata vikiwemo vishawishi mbalimbali ili niweze kupunguza kasi ya utendaji niliokuwanao lakini nilikuwa na msimamo wa kutekeleza majukumu yangu ya kikazi kwa haki kama nilivyoagizwa na viongozi wangu,” alisema Kombe.

Aliongeza kuwa hali hiyo iliashiria kujengeka kwa hali ya chuki kwa baadhi ya mitandao ya wafanya biashara mkoani humo waliokuwa wakijishughulisha na biashara mbalimbali zikiwemo za mafuta, sabuni, bati na nyinginezo  huku wakibainika kukwepa kulipa mapato ya serikali.
Aliendelea kusema kuwa katika mamlaka hiyo aliitumikia zaidi ya miaka 11 akiwa ameitumikia serikali kwa uaminifu hadi Februari, 1998 alipomwagiwa tindikali na watu wasiojulikana wakati akigonga katika geti la nyumba aliyokuwa akiishi eneo la Kirumba jijini Mwanza.

ANAIKUMBUKA SIKU HIYO YA BALAA
“Ilikuwa ni majira ya saa nne ya usiku nikiwa katika hali ya matembezi ya kawaida ambapo katika matembezi hayo walijitokeza baadhi ya wafanyabiashara ambao walinisalimia ndipo baada ya kuachana nao nilielekea nyumbani kwangu, nilipofika kwenye geti nilianza kugonga ili mlinzi aje afungue ghafla niliitwa jina langu na mtu niliyehisi alikuwa nyuma yangu, nilipogeuka, ghafla nilimwagiwa tindikali kichwani,” alisema Kombe.
Akaongeza kuwa tukio hilo lililoashiria kupangwa lilimletea maumivu makali ya kichwa ambapo alipelekwa Hospitali ya Rufaa ya Bugando Mwanza na baadaye akahamishiwa KCMC. Baada ya kushindikana katika hospitali hizo alipelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Leeds iliyopo nchini Uingereza kwa ajili ya matibabu zaidi ambapo baada ya miezi minane alipata nafuu na kurudi nchini.
Kombe ameshangazwa na hatua ya serikali kumlipa shilingi milioni 12 kama mafao yake huku ikiwa imemtelekeza kwa kumwachisha kazi wakati ana familia ya watoto wanne  wanaomtegemea na kwamba fedha hizo hazimtoshi kutokana na majeraha aliyoyapata katika eneo la kichwa na maeneo mengine ya mwili wake.
“Naiomba serikali inipatie kazi kwani ulemavu wangu hauwezi kunizuia kufanya kazi katika idara yoyote au katika mamlaka hiyo hata kama ni kitengo cha huduma kwa wateja, mawasiliano na nyinginezo ili  niweze kujipatia kipato cha kuniwezesha kuishi na familia yangu na kunisaidia katika matibabu.”
Yeyote aliyeguswa na habari hii anaweza kumsaidia mpiganaji huyu wa uchumi wa nchi hii kwa simu namba 0787 926549 Kutoa ni moyo.

Monday, September 23, 2013

KAMA HUIJUI HISTORIA YA AL SHABAAB BASI KARIBU UISOME HAPA UJE WALITOKEA WAPI HADI LEO WAMEKUA TISHIO

Kundi la wapiganaji wa kisomali la al-Shabaab,limevamia jumba la kifahari lenye maduka na mikahawa nchini Kenya. Al Shabaab lenya mizizi yake nchini Somalia, limeweza kuondolewa kutoka miji mikubwa ya Somalia ikiwemo Mogadishu na sehemu zengine za Somalia , ingawa bado linasalia kuwa tisho kubwa kwa kanda nzima.

Al Shabaab ni nani?

Jina Al-Shabab linamaanisha Kijana kwa lugha ya kiarabu. Kundi hilo liliibuka kama tawi la vijana la muungano wa mahakama za kiislmau ambao baadaye ulivunjika mwaka 2006, wakati ilipopigana na wanajeshi wa Ethiopia waliokuwa wameingia nchini Somalia kuunga mkono serikali iliyokuwa dhaifu.
Kuna taarifa chungu nzima kuhusu wapiganaji wa kiisilamu wanaokwenda Somalia kupigania Al Shabaab.
Kundi hilo limeweka sheria kali za kiisilamu katika maeneo ambayo linadhibiti ikiwemo kupigwa kwa mawe hadi kufa wanawake wanaodaiwa kufanya uasherati pamoja na kuwakata wezi mikono.

Je Al Shabaab linadhibiti sehemu gani ya Somalia?

Ingawa kundi hilo limepoteza udhibiti, wa miji mikubwa, bado linakita mizizi katika maeneo ya mashinani.
Lililazimika kuondoka katika mji mkuu Mogadishu, mwezi Agosti mwaka 2011 na pia kuondoka katika mji wa bandarini wa Kismayo mwezi Septemba mwaka 2012.
Kismayo ulikuwa mji muhimu kwa kundi hilo, ambao ulikuwa unawezesha bidhaa kuwafikia wapiganaji wa kundi hilo pamoja na kuwatoza watu ushuru kwa shughuli zao.
Hizi ni silaha za Al Shabaab walizonasa wanajeshi wa AU
Muungano wa Afrika, ambao unaunga mkono juhudi za majeshi ya serikali, ulisherehekea ushindi huo ingawa al-Shabab hunfanya mashambulizi ya mara kwa mara ya kujitoa mhanga mjini Mogadishu na kwingineko.
Wadadisi wanaamini kuwa al-Shabab limeanza kufanya mashambulizi ya kuvizia baada ya kushindwa na majeshi ya Muungano wa Afrika wanaotumia nguvu dhidi yao.
Lakini linakabiliwa na tisho kubwa kutoka kwa wanajeshi wa Kenya walianza hatarakti zao dhidi ya kundi hilo kuanzia mwaka 2011.
Kenya ilituhumu wapiganaji wa al-Shabab kwa kuwateka nyara wanajeshi wake pamoja na watalii na sasa wamekuwa katika msitari wa mbele kupambana na kundi hilo la kigaidi.
Wakati huo, wanajeshi wa Ethiopia waliweza kukabiliana na wapiganaji hao na kudhibiti miji ya Beledweyne na Baidoa.

Nani kiongozi wa al-Shabab?

Ahmed Abdi Godane ndiye kiongozi wa kundi hilo. Anajulikana kama Mukhtar Abu Zubair, na anatoka katika jimbo la Somaliland.
Kumekuwa na taarifa za mgawanyiko katika kundi hilo, ambazo hata hivyo zinapingwa vikali na kundi lenyewe. Inaarifiwa kuwa uongozi wake unapingwa, na wanachama wanaotoka maeneo ya Kusini na ambao ni wengi katika kundi hilo. Inakisiwa idadi yao ni kati ya wanajeshi 7,000 na 9,000.
Bwana Godane huwa haonekani hadharani . Mtangulizi wake Moalim Aden Hashi Ayro, aliuawa katika shambulizi lililofanywa na Marekani mwaka 2008.

Nini uhusiano wa kimataifa wa kundi hilo?

Al Shabaab wakifanya mashambulizi mjini Mogadishu
Al-Shabab lilijiunga na al-Qaeda mwezi Februari mwaka 2012. Katika ujumbe wa Video, kiongozi wa al-Shabab Ahmed Abdi Godane alisema anaahidi kuunga mkono kingozi wa al-Qaeda Ayman al-Zawahiri.
Makundi hayo mawili yamekuwa yakifanya kazi kwa pamoja, na raia wa kigeni wamekuwa wakiunga mkono kundi hilo, na hata kuwasaidia katika harakati zao za mapigano.
Mwaka jana maafisa wa al-Shabab waliambatana na mtu aliyesema ni mwanachama wa al-Qaeda na kumtambua kuwa raia wa Marekani Abu Abdulla Almuhajir alipokuwa anatoa msaada wa chakula kwa waathiriwa wa njaa.
Maafisa nchini Marekani wanaamini kuwa wapiganaji wa Al Qaeeda ambao hawajahusina sana na mashambulizi nchini Afghanistan na Pakistan kufuatia mauaji ya kiongozi wao,Osama bin Laden, wapiganaji wake wengi wanakwenda kutafuta hifadhi nchini Somalia

TAZAMA PICHA ZA SIMBA ALIE SUMBUA NA KUUWA MIFUGO MJINI MOROGORO BAADA YA KUULIWA..!!

Kwa kimombo tunaiita 'life and death', Simba aliyetumia fursa vizuri kwa kujilia mbuzi 47 ameyaonja mauti baada ya kupigwa hadi kufa na Askari wanyamapri.
Simba huyo ambaye amesumbua kwa muda mrefu Mkoani humo maaskari Wanyamapori Mkoani Morogoro wamemwinda na kumuua simba huyo aliyetafuna mbuzi 47 katika Mlima Uluguru eneo la kijiji cha Bagilo kata ya Kinole, Tarafa ya Mkuyuni Mkoani humo.



Askari wanyamapori Wakimchuna ngozi simba

SAMAHANI PICHA HII INATISHA;AJALI MBAYA YAMKUTA MWENDESHA PIKIPIKI MAARUFU KAMA ASSECDO NI MITAA YA MIEMBENI BUKOBA

Ajali mbaya yamkuta mwendesha pikipiki mjini bukoba maarufu kama Assecdo, na kupuata madhara ya majeraha makubwa kichwani na mkononi kama inavyo onekana katika picha.
Ni baada ya kupalamia ukuta wa duka la nyama lililopo mitaa ya miembeni Center usawa wa kutokea barabara ya bukoba sekondari
Mpaka anapelekwe hospital hali yake haikuwa nzuri,ni tukio la mchana wa jumamosi weekend hii.
hadi tunaingia mitamboni atujapata habari zaidi kuhusiana na tukio hili na ukweli ni kwamba hali ya biashara ni tete ndani ya Burchar hiyo .
Picha kwa hisani ya Mdau Jon Do Pesa na Bukoba wadau blog

PICHA YA KWANZA YA MSEMAJI WA AL-SHABAAAB AKIJIGAMBA KWA KUWAUA WANANCHI WA KENYA JANA AT THE MALL!!

Al-Shabab spokesperson Ali Mohamud Rage holds a news conference in Mogadishu, Somalia.

"NINA WAKE FEKI WENGI SANA HAPA MJINI".....MZEE MAJUTO.


Majuto anasema kuwa ana watoto tisa ingawa hakuwa tayari kuwazungumzia mama wa watoto hao zaidi ya kumwongelea mkewe wa sasa, Aisha Mbwana kwa kuwa wake zake aliozaa nao baadhi ya watoto kwa bahati mbaya walishafariki dunia.


Alisema kuwa yanapokuja masuala ya familia huwa anapenda azungumze mkewe na kwa ridhaa yake. Kwa mujibu wa Majuto anapenda aitwe mke halali kwa kuwa wake feki anao wengi kupitia michezo ya kuigiza na wengine wenye fikira potofu hutumia picha hizo kutengeneza habari za uongo.


Aisha anaizungumziaje familia yake

Kama kawaida ya wanawake wa Tanga ana lafudhi ya huko ambayo huvutia kuzungumza nao, anaanza kwa kunieleza kuwa alianza kuitwa mke halali wa nguli huyo wa sanaa za maigizo mwaka 1997, walipofunga ndoa .


Anasema kuwa alikutana na nguli huyo maeneo ya Buguruni, Dar es Salaam, ambako alikuwa akiishi na dada yake aliyekuwa kaolewa na rafiki yake mzee Majuto, 

‘Mwanachia’ (kwa sasa ni marehemu), ambaye walikuwa wakiigiza pamoja.

Anasema hakuwa na hili wala lile hadi alipoamua kuondoka na kurudi kwao maeneo ya Vingunguti, ambako ndiko walikokuwa wanaishi wazazi wake na kupewa taarifa kuwa posa imepelekwa kwa ajili yake.
Nilipoambiwa kuhusu hiyo posa sikufikiria kama atakuwa ni mzee Majuto kwa kuwa alikuwa ni kama shemeji yangu kutokana na kuwa karibu na shemeji yangu,” anasema Aisha ambaye ni mama wa watoto watatu.

Anaendelea kueleza kuwa siku ambayo wanafamilia walikutana na kumuuliza kama anamfahamu mchumba na kutajiwa jina kuwa ni Amri Athumani, aliuliza mara mbili kwa kuwa alikuwa hamfahamu huyo mtu hadi alipoambiwa kuwa ni King Majuto.

“Kwa mila za Wabondei mchumba wa kwanza anakubaliana na wazazi, halafu binti anapewa taarifa na kwa kuwa wazazi ni wakubwa inabidi binti akubali, na ndivyo ilivyokuwa kwangu nikakubali na kuolewa na Majuto,” anasema mama huyo.

Anaingia kwenye uigizaji kufuata nyayo za mumewe

Aisha anafafanuwa kuwa kabla ya kuolewa na Majuto hakuwa mwigizaji lakini baada ya kuolewa, mumewe huyo alimwingiza kwenye uigizaji na filamu ya kwanza kuigiza na mumewe huyo ni ‘Fukara hatabiriki’.

Mkewe huyo anasema kipindi hicho Majuto alikuwa anafanya kazi bila kuwa na kikundi zaidi ya wanafamilia, hivyo na yeye alikuwa mmoja wao akicheza kama mama na Majuto kama baba.

Sunday, September 22, 2013

SOMA HAPA ALICHOKISEMA DIVA KATIKA WEB YAKE, NI KUMHUSU PREZOO NA TATOO YA PREZOO ILIYOPO MKONONI MWA DIVA.


Hey Guys Pliz Kwa Heshima Zote na taadhima naomba msiwe mna comment about Huddah Or Prezzo in My Page. That Chapter is closed muda mrefu sana and matter of fact Dont need Drama. My Life seems to be Naturally . I never have plans for where it’s going to take me. Huwa nafuta na kujisikia vibaya nikiona mbaendelea comment about Prezzo. well The truth ni Kuwa My heart Belonged to another man and The Tattoo of his name katika Mkono wangu itakuwa removed yes …. working on that. I Respect him and he is such a good Person but pliz enough with his name on My Page….hope mmenielewa. love you all.
Hey Guys Pliz Kwa Heshima Zote na taadhima naomba msiwe mna comment about Huddah Or Prezzo in My Page. That Chapter is closed muda mrefu sana and matter of fact Dont need Drama. My Life seems to be Naturally . I never have plans for where it’s going to take me. Huwa nafuta na kujisikia vibaya nikiona mbaendelea comment about Prezzo. well The truth ni Kuwa My heart Belonged to another man and The Tattoo of his name katika Mkono wangu itakuwa removed yes …. working on that. I Respect him and he is such a good Person but pliz enough with his name on My Page….hope mmenielewa. love you all.

MEHRA OMARY: TAZAMA PICHA JINSI UWANJA WA NDEGE WA DAR ES SALAA...

MEHRA OMARY: TAZAMA PICHA JINSI UWANJA WA NDEGE WA DAR ES SALAA...: TAZAMA PICHA JINSI UWANJA WA NDEGE WA DAR ES SALAAM UTAVYOKUWA WA KISASA NA WAKUVUTIA MNO...!! Pamoja na kuzipata hizi picha kuna...

MEHRA OMARY: TAZAMA PICHA JINSI UWANJA WA NDEGE WA DAR ES SALAA...

MEHRA OMARY: TAZAMA PICHA JINSI UWANJA WA NDEGE WA DAR ES SALAA...: TAZAMA PICHA JINSI UWANJA WA NDEGE WA DAR ES SALAAM UTAVYOKUWA WA KISASA NA WAKUVUTIA MNO...!! Pamoja na kuzipata hizi picha kuna...

TAZAMA PICHA JINSI UWANJA WA NDEGE WA DAR ES SALAAM UTAVYOKUWA WA KISASA NA WAKUVUTIA MNO...!!


2Pamoja na kuzipata hizi picha kuna maswali unaweza kuwa nayo ikiwemo Idadi ya ndege zitakazoweza kuhudumiwa kwenye uwanja huu mpya? utamalizika lini? gharama yake na mengine…
Naambiwa ujenzi wa huu uwanja unaambatana na ujenzi wa viwanja vingine katika baadhi ya mikoa ya Tanzania ikiwemo 87.8 Mbeya, 88.1 Mwanza na 89.2 Kigoma.
3
4
5
6
7
8
 

SOURCE: MILLADAYO.COM

JEURI YA FEDHA..DIAMOND PLATNUM APACHIKA GRAMU 87.97 KIFUANI KWAKE ZA GOLD HIZI HAPA.



JAMAA MZIGO KANUNUA MALAYSIA BAADA YA SHOW YA JANA

HATIMAYE AL SHABAAB WATHIBITISHA KUHUSIKA NA TUKIO LA MAUAJI KENYA, SOMA STORY HAPA



Kundi la wanamgambo wa kiisilamu la Al shabaab nchini Somalia limedai kutekeleza mauaji ya watu zaidi ya thelathini nchini Kenya kwa mujibu wa taarifa za vyombo vya habari nchini Kenya ( Citizen TV) na pia kupitia kwa ukurasa wake wa Twitter.

Shirika la habari la Reuters pia limesema kuwa Al Shabaab linasema kwamba Kenya ilipuuza mara kwa mara vitisho vya kundi hilo kuishambulia.

Taarifa kutoka Ikulu ya Rais Kenya zinasema kuwa mshukiwa mmoja amekamatwa. Mshukiwa huyo amejeruhiwa na anapokea matibabu hospitalini.

Wanamgambo wa Al Shabaab wanasema kuwa Kenya haikuchukulia kwa uzito onyo walilotoa kwa taifa hilo kwa hatua ya kuwapeleka wanajeshi wake nchini humo kupambana dhidi yao.

Kundi hilo limesema limekuwa likitoa onyo mara kwa mara kwa Kenya kuwa ikiwa haitaondoa vikosi vyake nchini Somalia, athari zitakuwa mbaya mno.
Kupitia mtandao wao wa Twitter, Al Shabaab limesema kuwa Kenya ilijidai kutosikia onyo hizo, na kuendelea kuwaua waisilamu wasio na hatia nchini Somalia.

Taarifa hiyo ya Twitter ilisema kuwa Shambulio la Westgate ni tone katika bahari tu ya mfano wa yanayowakumba wasomali waisilamu nchini Somalia.

Taharuki ilianza hii leo saa saba mchana wakati watu wanaokisiwa kuwa kumi walipovamia jengo la kifahari la Westgate la kuwapiga risasi kiholela wakenya waliokuwa wanaendelea na shughuli zao za kawaida.

Kwa mujibu wa shirika la msalaba mwekundu , takriban watu 30 walifariki kwa kupigwa risasi au kutokana na majeraha yao na wengine wengi wenye majeraha ya risasi kukimbizwa hospitalini kwa matibabu.

-BBC

PICHA ZA KUSIKITISHA KATIKA SHAMBULIO LA KENYA HAPO JANA..!! TAHADHARI BAADHI YA PICHA ZINATISHA.!


September 21, ni tarehe ambayo Kenya haitoisahau kamwe. Ni baada ya kundi la wanamgambo wa Al-Shabab lilipoishambulia mall ya Westgate maarufu kwa kuwa na wateja matajiri jijini Nairobi na kuwashikilia watu mateka, kuwaua na kuwajeruhi wengine.
Mwanamke aliyekuwa amejeruhiwa akiomba msaada Mwanamke aliyekuwa amejeruhiwa akiomba msaada
Familia ikiwa imeshikana mikono wakati ikitoka nje ya eneo la hatari Familia ikiwa imeshikana mikono wakati ikitoka nje ya eneo la hatari
article-2427892-182485E800000578-152_964x631
130921145130-25-kenya-mall-restricted-horizontal-gallery
130921103725-07-kenya-mall-horizontal-gallery
Mashuhuda wanasema watu hao waliokuwa na silaha, wakiwa na nguo nyeusi na vichwa vyao vikifunikwa na vilemba waliingia kwenye mall hiyo ya Westgate jana mchana. Mpaka sasa, idadi ya watu walioshikiliwa mateka ndani ya mall hiyo haijajulikana.
Mama na wanae akiwa amejificha kuhofia kuuawa na watu hao makatili Mama na wanae akiwa amejificha kuhofia kuuawa na watu hao makatili
Mfanyakazi wa Red Cross akimbeba mtoto aliyekuwa ndani ya mall hiyo Mfanyakazi wa Red Cross akimbeba mtoto aliyekuwa ndani ya mall hiyo
Mtoto akikimbia kuokoa maisha yake Mtoto akikimbia kuokoa maisha yake
Mtoto akiwa nje baada ya kutolewa ndani ya mall, pembeni ni mwili wa mtu aliyeuawa
Mtoto akiwa nje baada ya kutolewa ndani ya mall, pembeni ni mwili wa mtu aliyeuawa

Zaidi ya watu 40 wameripotiwa kuuawa na zaidi ya 162 wakijeruhiwa.
Mtu na mpenzi wake waliouwa kwa pamoja na wanamgambo hao Mtu na mpenzi wake waliouwa kwa pamoja na wanamgambo hao
Mwanamke akilia kwa woga baada ya kuokolewa na askari Mwanamke akilia kwa woga baada ya kuokolewa na askari
Mwanamke aliyejeruhiwa akitolewa nje kwa kubebwa kwenye toroli la kufanyia shopping Mwanamke aliyejeruhiwa akitolewa nje kwa kubebwa kwenye toroli la kufanyia shopping
Mwanamke aliyekuwa ameshikiliwa mateka akiwa haamini baada ya kuachiwa Mwanamke aliyekuwa ameshikiliwa mateka akiwa haamini baada ya kuachiwa
Maafisa wamesema watu hao wamebananishwa na kwamba watu wameshikiliwa mateka kwenye maeneo mbalimbali. Al-Shabab imeliambia shirika la habari la Uingereza BBC kuwa limefanya shambulio hilo kujibu opereshini za kijeshi za Kenya zinazoendelea nchini Somalia.
<img src="http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2013/09/Mwanaume-aliyejeruhiwa-akilia-kwa-uchungu-kutokana-na-maumivu-makali-baada-ya-kupigwa-risasi-ya-mguu.jpg" alt="Mwanaume aliyejeruhiwa akilia kwa uchungu kutokana na maumivu makali baada ya kupigwa risasi ya mguu" width="600" height="400" class="aligncenter size-full wp-image-57459" Mwanaume aliyejeruhiwa akilia kwa uchungu kutokana na maumivu makali baada ya kupigwa risasi ya mguu
Ofisa wa usalama na wenzake wakielekezana na wenzake mahali walipo watu hao wenye silaha Ofisa wa usalama na wenzake wakielekezana na wenzake mahali walipo watu hao wenye silaha
Polisi akisaidia kumtoa mtoto aliyekuwa ndani ya mall Polisi akisaidia kumtoa mtoto aliyekuwa ndani ya mall
Polisi na wanajeshi wakipambana na magaidi hao Polisi na wanajeshi wakipambana na magaidi hao
Mashuhuda wengine wamedai kuwa wanamgambo hao waliwaambia waislamu waondoke na wabaki waumini wa dini zingine.
“Walisema na kusema: ‘Kama wewe ni muislamu, simama. Tumekuja kuwaokoa,” Elijah Lamau aliiambia BBC. Alisema waislamu waliondoka wakiwa wamenyoosha mikono juu na kisha watu hao wakawapiga risasi watu wawili.
Polisi wa Kenya akiwa ameshika tumbo lake baada ya kujeruhiwa huku mwenzake akiendelea kurushiana risasi na magaidi wa Al-Shabab Polisi wa Kenya akiwa ameshika tumbo lake baada ya kujeruhiwa huku mwenzake akiendelea kurushiana risasi na magaidi wa Al-Shabab
Polisi wakiingia ndani ya mall hiyo kupambana na wana mgambo wa Al-Shabab Polisi wakiingia ndani ya mall hiyo kupambana na wana mgambo wa Al-Shabab
Polisi wakipambana na Al-shabab Polisi wakipambana na Al-Shabab
Rais wa Canada Annemarie Desloges, 29, aliuawa kwa risasi na magaidi hao Raia wa Canada Annemarie Desloges, 29, aliuawa kwa risasi na magaidi hao
Wanajeshi walimwaga kwenda kusaidia kupambana na watekaji wa kundi la kigaida la Al-shabab Wanajeshi walimwaga kwenda kusaidia kupambana na watekaji wa kundi la kigaida la Al-Shabab
Wananchi wa mataifa mbalimbali waliokuwa wakifanya shopping kwenye mall hiyo wakiwambia kuinua mikono yao kuonesha hawana silaha Wananchi wa mataifa mbalimbali waliokuwa wakifanya shopping kwenye mall hiyo wakiwambia kuinua mikono yao kuonesha hawana silaha
Gaidi mmoja alikamatwa jana na kufa kutokana na majeraha. Maafisa wa Kenya wameimbia BBC kuwa wengine wanne wamekamatwa. Wananchi wakikimbia kuokoa maisha yao Wananchi wakikimbia kuokoa maisha yao
Wanawake na watoto wao wakihaha kuokoa maisha yao ndani ya mall hiyo Wanawake na watoto wao wakihaha kuokoa maisha yao ndani ya mall hiyo
Wanawake waliojeruhiwa wakisaidiwa Wanawake waliojeruhiwa wakisaidiwa
Watu mbalimbali wakijaribu kuokoa maisha yao wakati watu hao wenye silaha wakiwa ndani ya mall Watu mbalimbali wakijaribu kuokoa maisha yao wakati watu hao wenye silaha wakiwa ndani ya mall
Watu wakimsaidia kumdaka msichana aliyekuwa amejificha ndanii ya mall hiyo Watu wakimsaidia kumdaka msichana aliyekuwa amejificha ndanii ya mall hiyo
Watu wakisaidiwa kutoka nje ya mall, pembeni ni mwili wa mtu aliyeuawa Watu wakisaidiwa kutoka nje ya mall, pembeni ni mwili wa mtu aliyeuawa
Watu waliokuwa ndani ya Westgate wakisaidiwa kutoka nje na askari Watu waliokuwa ndani ya Westgate wakisaidiwa kutoka nje na askari
Watu waliokuwa wakifanya shopping wakisaidiwa kutoka nje ya mall na askari Watu waliokuwa wakifanya shopping wakisaidiwa kutoka nje ya mall na askari