Wednesday, February 27, 2013

PICHA  15 ZA KILICHOJIRI KATIKA MAZISHI YA ALIYEKUA MCHUMBA WA PREZOO

DSC_0320

DSC_0376
DSC_0379
DSC_0317
DSC_0400
DSC_0510
DSC_0392
Goldie's husband, Andrew Harvey
Picture 15
Goldie casket
Goldie's burial
May Goldie’s soul rest in eternal peace

Monday, February 25, 2013

HII NDIO SHULE ILIYOSHIKA NAFASI YA MWISHO KITAIFA KATIKA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE




MATOKEO ya Mtihani wa Kidato cha Nne mwaka 2012 yaliyotangazwa mwanzoni mwa juma, yanaendelea kutawala mijadala mbalimbali kila kona.

Sababu kubwa ya mijadala hiyo kutawala yaweza kuwa ni
takriban kila familia kuguswa kwa njia moja ama nyingine na matokeo hayo.

Katika matokeo hayo karibu shule zote za umma zimefanya vibaya, zile za kata zikiongoza katika kufelisha, huku ile ya Mibuyuni iliyopo Kilwa mkoani Lindi ikiwa ya mwisho kabisa katika kundi la shule zenye zaidi ya wanafunzi 40.

Mkuu msaidizi wa shule hiyo Robart Mzumbi, alisema kuwa matokeo hayo yalitarajiwa kwa kuwa tangu wanafunzi hao walipoandikishwa kidato cha kwanza, hawakuwa wamefaulu.

Alibainisha kuwa, matokeo ya kidato cha pili ya wanafunzi hao walipofanya mtihani wa taifa mwaka 2010, yalikuwa kiashiria kingine kwamba, hata kwenye matokeo ya mtihani wa kidato cha nne wanafunzi hao hawatafanya vizuri.

Pamoja na hayo, Mzumbi anaeleza kwamba kwa kuwa lengo lao lilikuwa ni kuhakikisha wanafundisha watoto hao na mwisho wafanye vyema, matokeo hayo yamewasikitisha kwa kiasi kikubwa.

Alitaja upungufu wa walimu na umaskini wa kipato kwa jamii inayozunguka shule hiyo kuwa ni moja ya sababu kubwa zilizosababisha matokeo hayo mabaya.


Mwalimu huyo alibainisha kwamba idadi kubwa ya wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo hujishughulisha zaidi na biashara ndogo ndogo, badala ya kusoma.

Aliweka wazi kuwa, shule hiyo ilikuwa ya mwisho kati ya shule 3,392 zenye watahiniwa 40 na kuendelea, wakati watahiniwa hao wa mwaka 2012 walipochaguliwa kuingia kidato cha kwanza mwaka 2009, ambapo walikuwa na alama za chini.

Aliongeza kuwa wanafunzi hao walichaguliwa kuanza kidato cha kwanza wakati tayari wengi wao walishaanza kufanya biashara ndogondogo, hivyo walikusanywa kutoka huko mitaani na kupelekwa shule.

“Ndugu yangu shule yetu huwa inafanya vizuri kidogo, angalia matokeo ya kidato cha pili mwaka huu Sekondari ya Mibuyuni imekuwa ya 115 kati ya shule 242 za Kanda ya Kusini, wanafunzi wanane wamefaulu kati ya 25 waliofanya mtihani. Lakini kwa matokeo ya kidato cha nne, kwa kweli wanafunzi waliochaguliwa mwaka 2009, hawakuwa na sifa bali waliokotwa tu ili kujaza darasa,” alisema na kuongeza:

“Hata mtihani wa kidato cha pili mwaka 2010, walifanya vibaya sana na shule hii ilikuwa ya pili kutoka mwisho.”

Mzumbi alisema kwamba shule hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwamo kukosa maabara, upungufu wa walimu wa sayansi, usafiri na umeme wa uhakika.

Pia ina ukosefu wa maji, nyumba za walimu, mabweni kwa ajili ya watoto wa kike, pamoja na shule kujengwa mbali na makazi ya wananchi.

Alieleza kuwa wanafunzi wengi wanaosoma katika shule mbalimbali za Mkoa wa Lindi, hulazimika kutembea umbali mrefu kutoka nyumbani kwenda shuleni.
source:mwananchi.co.tz

KWA SHABIKI WA DOGO JANJA, CHECK OUT PICHA ZA DOGO JANJA AKIWA SOUTH AFRIKA


Msanii kutoka Arusha ambae kwa sasa makazi yake yamehamia Bongo, akiwa chini ya label ya Watanashati Entertainment akiwa kishule na kimuziki zaidi, Dogo Janja yupo jijini Cape Town, South Africa.
 
Janjaro ambae kwa sasa anatamba na ngoma yake inayokwenda kwa jina la Ya Moyoni akimshirikisha Mtanashati mwenzie, PNC bado haijafahamika kuwa ameenda nchini humo kwa ajili ya matembezi au kwa shughuli za kimuziki.

Bado tunafuatilia kwa karibu ili kujua kilichompeleka huko.

PICHA YA SIKU YA LEO - KATIKATI YA MBUGA HIACE NA TEMBO

TEMBO AKIJERUHI GARI AINA YA HIACE

TIMBULO KAKAMATWA BURUNDI NA MADAWA YA KULEVYA?



Kuna tetesi kuwa msanii wa Bongo flava maarufu kwa jina la Timbulo, ambaye amepata umaarufu mkubwa kutokana na umahiri wa kuimba katika nyimbo zake kadhaa kama  Domo Langu, Waleo Wakesho, Samson na Delilah, amekamatwa mjini Bujumbura kwa tuhuma za kukutwa na madawa ya kulevya. Timbulo alikuwa huko katika kufanya mipango ya kufanya maonyesho kadhaa nchini Burundi mwezi April mwaka huu

Sunday, February 24, 2013


                                AJALI NYINGINE MKOANI IRINGA

 Hii ni ajali ya  pili    kutokea usiku  wa leo katika Manispaa ya Iringa imetokea eneo la Kitwiru baada ya  lori  lililobeba mbao kuacha njia na kugonga nguzo ya umeme kabla ya  kuanguka ,hakuna  aliyepoteza maisha wala  majeraha ya  kutisha

 Hii ni nguzo ya umeme na kibanda  kilichogongwa na lori hilo
Shehena ya  mbao  zikiwa  zimemwagika baada ya ajali  hii

Saturday, February 23, 2013

KAHABA AJIFUNGUA, AUA KICHANGA, CHEKI PICHA HAPA



Afisa polisi akikiokota kichanga hicho kilicho tupwa na kahaba
Stori:Dustani Shekidele, Morogoro
MTOTO mchanga hivi karibuni ametupwa katika Mto Kikundi mjini hapa akiwa amekufa, jirani kabisa na kambi ya makahaba wanaofanya biashara ya kuuza miili yao ‘machangudoa’. Baadhi ya watu walioshuhudia mwili wa kichanga hicho walimwambia mwandishi wetu kuwa kichanga hicho kilitupwa na mmoja wa makahaba, hali iliyozua tafrani kwani wasichana wanaoaminika kuwa ni makahaba walikuwa wakiipinga kauli hiyo.
“We mpigapicha usiamini hayo wanayosema hao watu... tuna ujinga kiasi gani tuzae, tuue kisha tutupe mtoto sehemu yetu ya kazi?” alihoji msichana mmoja ambaye alikataa kujitambulisha.
Hata hivyo, wasichana waliojitambulisha kwa majina Pendo Komba, Rose Joseph na Amanda Athuman kwa nyakati tofauti walisema wanaofanya unyama huo ni makahaba japokuwa wenyewe wanakataa.
Walidai kuwa hii ni mara ya sita kwa watoto wachanga kutupwa kwenye eneo hilo.
Afisi mmoja wa polisi aliyekuwepo eneo hilo, (jina tunalihifadhi) wakati wanauchukua mwili wa kichanga hicho alisema wanamtafuta mwanamke aliyefanya ukatili huo ili afikishwe mahakamani.

GARI LA KANUMBA LAMSHINDA DK. CHENI, SASA LIPO SOKONI KWA MIL 40


Habari za ndani kutoka kwa chanzo chetu zinasema kwamba, mteja aliyekuwa akitegemewa zaidi ni msanii maarufu nchini, Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’ ambaye baada ya kutajiwa bei alipewa kwa ajili ya kulifanyia majaribio.
CHANZO KINATIRIRIKA
Kwa sharti la kutochorwa jina lake gazetini chanzo hicho kilitiririka kuwa, si kweli kuwa Dk. Cheni alipewa lile gari ili alitumie kwa muda kufanya vifaa visiharibike bali alikuwa akilijaribu.
“Unajua ndugu yangu lile gari wenyewe (familia ya Kanumba) wanaliuza milioni 40, Cheni amelikagua sana akagundua lina matatizo mengi ndiyo maana akawaambia atoe milioni 25 wamekataa na sasa limemshinda na ameshalirudisha,” kilipasha chanzo.
 
Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’.
MATATIZO YENYEWE
Kikiendelea kutambaa na mistari, chanzo hicho kilitaja baadhi ya matatizo ya gari hilo, kikasema: “Kwanza namba zake za usajili ni za zamani ni T 750 AER, gia boksi ina matatizo ambayo yamesababishwa na gari hilo kutumika likiwa kwenye four wheel ndiyo maana gia boksi imepata matatizo.
“Halina motor vehicle,  steeling power mbovu, halina road licence na mbaya zaidi kwa namna lilivyo kwa mizunguko ya kawaida mjini, kwa siku linatumia mafuta ya laki moja.
Vyote hivi Dk. Cheni aliviorodhesha na kwenda kuwaeleza ili wapunguze bei lakini wamegoma, wanataka milioni 40 wakati Cheni ameng’ang’ania kuwa anataka kutoa 25 (milioni).”
DK. CHENI KIZIMBANI
Baada ya kupata maelezo haya kutoka kwa chanzo, Ijumaa lilimvutia waya Dk. Cheni na kumuuliza juu ya madai hayo, alisikiliza kwa makini sana maelezo yote hadi mwisho, alipotakiwa kujibu, akakata simu kisha akazima kabisa.