BREAKING NEWS....NYUMBA YATEKETEA KWA MOTO WA KIMIUJIZA IRINGA
Mkazi wa Zizi la Ng'ombe kata ya Isakalilo mjini Iringa Juma Said ( kushoto) akiwa na askari wa jeshi la Zimamoto na uokoaji mkoa wa Iringa na askari wa upelelezi wakitazama vifaa vyake vya muziki ambavyo zimeteketea kwa moto mchana wa leo
Askari wa Zimamoto na wakikusanya mabaki ya mali za mkazi huyo baada ya kuteketea kwa moto
Askari wa jeshi la Zimamoto na uokoaji mkoa wa Iringa (kulia) wakimshauri mkazi wa Zizi la Ng'ombe kata ya Isakalilo mjini Iringa Juma said kushoto kutoa nje ya nyumba mali zake zote zilizoteketea kwa moto ili kuzima kuhakiki moto zaidi
Wananchi wa Isakalilo wakitazama nyumba ambayo ilikuwa ikiteketea kwa moto kimiujiza
Mali zilizoteketea kwa moto
Magari ya Zimamoto yakiwa kazini leo
Magari ya Zimamoto na lile la jeshi la polisi wakiwa katika eneo la tukio
Mali zilizoteketea moto leo
Bw Juma Said akikusanya mabaki ya mali zilizosalia katika tukio hilo la moto
MOTO mkubwa uliowaka kimiujiza umetetekeza nyumba na mali mali mbali mbali zilizokuwemo katika nyumba ya mkazi wa mtaa wa Izizi la Ng'ombe kata ya Isakalilo katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Bw .Juma Said.
Tukio hilo limetokea leo majira ya saa 6.38 mchana wakati mmiliki wa nyumba hiyo akiwa katika shughuli nyingine za kikazi mbali na eneo hilo la Zizi la Ng'ombe.
Wakizungumza na mwandishi wa mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com eneo la tukio baadhi ya mashuhuda walisema kuwa wameshangazwa kuona moto mkubwa ukiwaka katika paa la nyumba hiyo ambayo ilikuwa haina mtu yeyote.
Alisema mmoja kati ya mashuhuda Sarah Sanga kuwa baada ya kuona moto ukiwaka juu ya paa la nyumba walilazimika kufika eneo hilo na kutaka kujua kama moto huo unatoka katika nyumba hiyo ama ni nyasi zimechomwa jirani na nyumba hiyo.
Hata hivyo alisema baada ya kufika jirani na nyumbani hiyo ndipo walipobaini kuwa katika nyumba hiyo hakukuwa na mtu na milango yote ilikuwa imefungwa na ndipo walipoamua kuanza kuzima moto huo kwa kumwagia maji huku baadhi yao wakiwasiliana na jeshi la zimamoto na uokoaji mkoa wa Iringa ambao walifika haraka eneo hilo na kufanikiwa kuvunja milango ya nyumba hiyo na kuzima moto mkubwa ambao tayari ulikuwa umeshika kasi zaidi.
Ally Omary alisema kuwa hakuna mwananchi ambae anatambua chanzo cha moto huo kutokana na nyumba hiyo haikuwa na umeme wa Tanesco zaidi ya umeme wa genereta ambalo pia lilikuwa limezimwa.
"Tunapenda kuwapongeza sana hawa watu wa zimamoto Iringa kwa kufika haraka zaidi tena wakiwa na magari mawili na kusaidia kuzima moto huo vinginevyo madhara ambayo yangejitokeza yawezekana yangekuwa makubwa zaidi ikiwa ni pamoja na nyumba za jirani kushika moto"
Mmiliki wa nyumba hiyo Juma Said alisema kuwa moto huo ulianzia chumbani kwake ambako kulikuwa na mali mbali mbali vikiwemo vyombo vya muziki na mali nyingine nyingi ambazo zote zimeteketea .
Said alisema kuwa moto huo unaonyesha umeanzia kuwaka katika radio kutokana na jinsi ambazo mazingira yanaonyesha na kuwa hadi sasa thamani ya mali zote na uharibifu uliojitokeza bado kufahamika.
" Kweli nashindwa kujua moto huu ndani ya radio umeingiaje kwani ninavyoondoka radio ilikuwa haifanyi kazi na nyumba haina umeme zaidi ya Genereta ambayo huwa inawashwa usiku"
Diwani wa kata ya Isakalilo Bernad Kanika alisema mmiliki wa nyumba hiyo ambae amejeruhiwa kutokana na jitihada za kuvunja vioo kwa mikono amepelekwa kutibiwa huku akidai kuwa chanzo cha moto huo bado hakifahamiki kutokana na mazingira yanavyoonyesha.
Mkuu wa kituo cha jeshi la Zimamoto na uokoaji mkoa wa Iringa John Chadewa alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwa jitihada zao na zile za wananchi wa eneo hilo zimeweza kusaidia kuzima moto huo huku akisema changamoto kubwa ni ujenzi holela ambao wananchi wamekuwa wakijenga hadi katika barabara na kukwamisha gari ya zimamoto kupita kwa urahisi zaidi.
Askari wa Zimamoto na wakikusanya mabaki ya mali za mkazi huyo baada ya kuteketea kwa moto
Askari wa jeshi la Zimamoto na uokoaji mkoa wa Iringa (kulia) wakimshauri mkazi wa Zizi la Ng'ombe kata ya Isakalilo mjini Iringa Juma said kushoto kutoa nje ya nyumba mali zake zote zilizoteketea kwa moto ili kuzima kuhakiki moto zaidi
Wananchi wa Isakalilo wakitazama nyumba ambayo ilikuwa ikiteketea kwa moto kimiujiza
Mali zilizoteketea kwa moto
Magari ya Zimamoto yakiwa kazini leo
Magari ya Zimamoto na lile la jeshi la polisi wakiwa katika eneo la tukio
Mali zilizoteketea moto leo
Bw Juma Said akikusanya mabaki ya mali zilizosalia katika tukio hilo la moto
MOTO mkubwa uliowaka kimiujiza umetetekeza nyumba na mali mali mbali mbali zilizokuwemo katika nyumba ya mkazi wa mtaa wa Izizi la Ng'ombe kata ya Isakalilo katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Bw .Juma Said.
Tukio hilo limetokea leo majira ya saa 6.38 mchana wakati mmiliki wa nyumba hiyo akiwa katika shughuli nyingine za kikazi mbali na eneo hilo la Zizi la Ng'ombe.
Wakizungumza na mwandishi wa mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com eneo la tukio baadhi ya mashuhuda walisema kuwa wameshangazwa kuona moto mkubwa ukiwaka katika paa la nyumba hiyo ambayo ilikuwa haina mtu yeyote.
Alisema mmoja kati ya mashuhuda Sarah Sanga kuwa baada ya kuona moto ukiwaka juu ya paa la nyumba walilazimika kufika eneo hilo na kutaka kujua kama moto huo unatoka katika nyumba hiyo ama ni nyasi zimechomwa jirani na nyumba hiyo.
Hata hivyo alisema baada ya kufika jirani na nyumbani hiyo ndipo walipobaini kuwa katika nyumba hiyo hakukuwa na mtu na milango yote ilikuwa imefungwa na ndipo walipoamua kuanza kuzima moto huo kwa kumwagia maji huku baadhi yao wakiwasiliana na jeshi la zimamoto na uokoaji mkoa wa Iringa ambao walifika haraka eneo hilo na kufanikiwa kuvunja milango ya nyumba hiyo na kuzima moto mkubwa ambao tayari ulikuwa umeshika kasi zaidi.
Ally Omary alisema kuwa hakuna mwananchi ambae anatambua chanzo cha moto huo kutokana na nyumba hiyo haikuwa na umeme wa Tanesco zaidi ya umeme wa genereta ambalo pia lilikuwa limezimwa.
"Tunapenda kuwapongeza sana hawa watu wa zimamoto Iringa kwa kufika haraka zaidi tena wakiwa na magari mawili na kusaidia kuzima moto huo vinginevyo madhara ambayo yangejitokeza yawezekana yangekuwa makubwa zaidi ikiwa ni pamoja na nyumba za jirani kushika moto"
Mmiliki wa nyumba hiyo Juma Said alisema kuwa moto huo ulianzia chumbani kwake ambako kulikuwa na mali mbali mbali vikiwemo vyombo vya muziki na mali nyingine nyingi ambazo zote zimeteketea .
Said alisema kuwa moto huo unaonyesha umeanzia kuwaka katika radio kutokana na jinsi ambazo mazingira yanaonyesha na kuwa hadi sasa thamani ya mali zote na uharibifu uliojitokeza bado kufahamika.
" Kweli nashindwa kujua moto huu ndani ya radio umeingiaje kwani ninavyoondoka radio ilikuwa haifanyi kazi na nyumba haina umeme zaidi ya Genereta ambayo huwa inawashwa usiku"
Diwani wa kata ya Isakalilo Bernad Kanika alisema mmiliki wa nyumba hiyo ambae amejeruhiwa kutokana na jitihada za kuvunja vioo kwa mikono amepelekwa kutibiwa huku akidai kuwa chanzo cha moto huo bado hakifahamiki kutokana na mazingira yanavyoonyesha.
Mkuu wa kituo cha jeshi la Zimamoto na uokoaji mkoa wa Iringa John Chadewa alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwa jitihada zao na zile za wananchi wa eneo hilo zimeweza kusaidia kuzima moto huo huku akisema changamoto kubwa ni ujenzi holela ambao wananchi wamekuwa wakijenga hadi katika barabara na kukwamisha gari ya zimamoto kupita kwa urahisi zaidi.
No comments:
Post a Comment